The Book of Common Prayer
United States England Scotland Ireland Wales Canada World

    Kitabu cha Sala za Kanuni (1918)
The Zanzibar Book of Common Prayer in Swahili

 

KAWAIDA YA MARIAMU MB.

ZABURI Sehemu B, na Antifona zake.

Hizi zitumike Sikukuu tu; siku nyingine zitumike Zaburi na Antifona za kawaida.

Asubuhi: WIMBO 43.
Jioni: WIMBO 42.

Sala

Ee Bwana, utujalie, sisi watumishi wako neema yako ya mbinguni: Ibada za Sikukuu hii ya . . . Mariamu, Bikira Mbarikiwa, zitupatie amani nyingi; kwa maana kuzaa kwake kulituletea Mwokozi wetu. Kwa Yeye.

au sala iliyohusika.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Ee Yesu, Mwana wa Bikira,
    Twakutolea sifa zetu;
Pamoja naye Mungu Baba,
    Na Mungu Roho Mtakatifu. Amin.

SOMO. Tazama, bikira atachukua mimba, naye atazaa mwana, nao watamwita Jina lake Imanueli.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Bwana amemchagua tangu mwanzo.
    R. Bwana amemchagua tangu mwanzo.
    V. Amemkaribisha akae kwake.
    R. Tangu mwanzo.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Bwana amemchagua tangu mwanzo.
    V. Neema imemiminiwa midomoni mwako.
    R. Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele
 

Common of St. Mary

 

Translations of some common words:

  Zab., Zaburi: Psalm(s)
  Wimbo: Hymn
  Sala: Prayer or Collect
  Sala ya Asubuhi: Morning Prayer
  Sala ya Adhuhuri: Noontime Prayer
  Sala ya Jioni: Evening Prayer
  Sala ya Usiku: Night Prayer or Compline
  Sala ya Ukumbusho wa ...: Memorial Prayer of ...
  Bwana: Lord
  Somo: Lesson
  Baba yetu: Our Father (Lord's Prayer)
  Ant.: Antiphon

WAKATI WA PASAKA

ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya

Sala ya Adhuhuri

    VIITIKIO hivi,
    V. Bwana amemchagua tangu mwanzo. Haleluya. Haleluya.
    R. Bwana amemchagua tangu mwanzo. Haleluya. Haleluya.
    V. Amemkaribisha akae kwake.
    R. Haleluya. Haleluya.
    V. Atukuzwe, etc,
    R. Bwana amemchagua tangu mwanzo. Haleluya. Haleluya
    V. Neema imemiminiwa midomoni mwako. Haleluya.
    R. Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele Haleluya.
 


  

Easter Season

KAWAIDA YA MTUME

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, Kama nilivyowapenda ninyi.
    ZABURI Sehemu C. (Sikukuu tu).
    WIMBO 44.
    SALA iliyojusika.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, Wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
    WIMBO 44.

Sala ya Adhuhuri

SOMO. Kwa mikono ya mitume zilifanyika ishara na maajabu mengi katika watu.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Sauti yao imeenea duniani mwote.
    R. Sauti yao imeenea duniani mwote.
    V. Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu.
    R. Duniani mwote.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Sauti yao imeenea duniani mwote.
    V. Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote.
    R. Jina lako watalifanya kuwa kumbukumbu, Ee BWANA.
 

Common of a Prophet

WAKATI WA PASAKA

ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
ZABURI. Sehemu C. (Sikukuu tu.)
WIMBO 45.
SALA iliyohusika.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Ahimidiwe Mungu Baba,
    Na Mwana mwenye kufufuka,
Na Roho Mfariji naye,
    Zamani, leo, na milele. Amin.

    SOMO. Twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao, katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Mfurahieni BWANA, enyi Watakatifu wenye haki. Haleluya. Haleluya.
    R. Mfurahieni BWANA, enyi Watakatifu wenye haki. Haleluya. Haleluya.
    V. Mungu amewachagua ninyi kuwa urithi wake.
    R. Haleluya. Haleluya.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Mfurahieni BWANA, enyi Watakatifu wenye haki. Haleluya. Haleluya.
    V. Nuru ya daima itawaangaza Watakatifu wako, BWANA. Haleluya.
    R. Nao watapata uzima wa milele, Haleluya
 


 

Easter Season

KAWAIDA YA MTAKATIFU

ZABURI na Antifona za kawaida.
WIMBO uliohusika.
SALA iliyohusika (taz. uk. 121-123).

Sala ya Adhuhuri

    SOMO. Baraka na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu zina Mungu wetu hata milele na milele. Amin.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Wenye haki hufurahi usoni pa Mungu.
    R. Wenye haki hufurahi usoni pa Mungu.
    V. Naam, hupiga kelele kwa furaha.
    R. Usoni pa Mungu.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Wenye haki hufurahi usoni pa Mungu.
    V. Wenye haki waishi milele.
    R. Na thawabu yao i katika Bwana.
 

Common of a Saint

WAKATI WA PASAKA

ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Ahimidiwe Mungu Baba,
    Na Mwana mwenye kufufuka,
Na Roho Mfariji naye,
    Zamani, leo, na milele. Amin.

    VIITIKIO hivi,
    V. Wenye haki hufurahi usoni pa Mungu. Haleluya. Haleluya.
    R. Wenye haki hufurahi usoni pa Mungu. Haleluya. Haleluya.
    V. Naam, hupiga kelele kwa furaha.
    R. Haleluya. Haleluya.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Wenye haki hufurahi usoni pa Mungu. Haleluya Haleluya.
    V. Wenye haki waishi milele. Haleluya.
    R. Na thawabu yao i katika Bwana. Haleluya.
 

Easter Season

SALA ZA KAWAIDA

(1) Mkesha wa Mtume

Mwenyezi Mungu, tunakuomba, utujalie rehema zako: Tuifurahie Sikukuu ya N. Mtume wako Mbarikiwa; ili tusaidiwe kwa sala zake, na kuokoka na hatari zote. Kwa.
 

Collects

Vigil of a Prophet

(2) Shahidi aliye Askofu

Mwenyezi Mungu, uuangalie udhaifu wetu: Utujalie tusaidiwe kwa sala tukufu za N. Mbarikiwa, Shahidi wako na Askofu; kwa kuwa tunalemewa na mzigo wa dhambi zetu. Kwa.
 

Martyred Bishop

(3) Shahidi asiye Askofu

Mwenyezi Mungu, tunakuomba, utujalie baraka zako: Tuiadhimishe vema Sikukuu hii ya N. Shahidi wako Mbarikiwa; ili tusaidiwe kwa sala zake, na kuzidi kulipenda Jina lako. Kwa.
 

Marty who was not a Bishop

(4) Mashahidi wengi

Mwenyezi Mungu, umetujalia kuiadhimisha Sikukuu ya N. na N., Mashahidi wako Wabarikiwa: Tunakusihi utuonyeshe rehema zako; ili tufurahi pamoja nao katika utukufu wako wa milele. Kwa.

(5) (Wakati wa Pasaka)
Kama 2 au 3.
(6) (Wakati wa Pasaka)
Kama 4.
 

Many Martyrs

(7) Mwungamaji aliye Askofu

Mwenyezi Mungu, tunakuomba, Sikukuu hii ituletee baraka zako: Tumwadhimishe N. Mbarikiwa, Mwungamaji wako na Askofu; ili tuzidi kukupenda, tukajaliwe wokovu wa milele. Kwa.
 

A penitent Bishop

(8) Mwalimu wa Dini. I

Ee Bwana, tunakusihi, uzisikie sala zetu: Tunazo-kutolea katika Sikukuu hii ya N. Mbarikiwa, Askofu wako na Mwalimu wa Dini; na kwa kuwa astahili kukuhudumia, kwa kuombea kwake utusamehe dhambi zetu zote. Kwa.

(9) Mwalimu wa Dini. II

Mwenyezi Mungu, umemweka N. Mwalimu wako Mbarikiwa awahudumie watu wako uzima wa milele: Utusikie tunakusihi; sisi tulioelimishwa naye hapa duniani, tuzidi kuombewa naye huko mbinguni. Kwa.
 

A Teacher of the Faith

(10) Mwungamaji asiye Askofu

Ee Mungu, watufurahisha kila mwaka kwa sifa njema za N. Mwungamaji wako Mbarikiwa: Utujalie tunakuomba; ili tuiadhimishe vema Sikukuu yake, na kumfuatisha mwenendo wake. Kwa.
 

A Penitent who was not a Bishop

(11) Mtauwa

Ee Bwana, tunakusihi: Tuombewe na N. Mtauwa mkuu Mbarikiwa; ili kwa sala zake tuone kibali kwako, kwa maana stahili zetu hazifai neno. Kwa.
 

 
A Monastic

(12) Bikira aliye Shahidi

Mwenyezi Mungu, Mfanya miujiza yote, ulipenda wanawake wamshinde adui wetu kwa kufa kishahidi: Utujalie tuiadhimishe vema Sikukuu ya N. Bikira na Shahidi wako Mbarikiwa; ili tumfuatishe mwenendo wake, na kukufikia Wewe salama. Kwa.
 

 
A virgin Martyr

(13) Bikira asiye Shahidi

Utusikie, Ee Mungu wa wokovu wetu: Tuifurahie Sikukuu hii ya N. Bikira wako Mbarikiwa; na kuelimishwa hali ya utauwa lia upendo. Kwa.
 

A Virgin not a Martyr

(14) Mwanamke aliye Shahidi

Mwenyezi Mungu, Mfanya miujiza yote, ulipenda wanawake wamshinde adui wetu kwa kufa kishahidi: Utujalie tuiadhimishe vema Sikukuu ya N. Shahidi wako Mbarikiwa; ili tumfuatishe mwenendo wake, na kukufikia Wewe salama. Kwa.
 

A female Martyr

(15) Mwanamke asiye Shahidi

Utusikie, Ee Mungu wa wokovu wetu: Tuifurahie Sikukuu hii ya N. Mtakatifu wako; na kuelimishwa hali ya utauwa na upendo. Kwa.

 

A Woman not a Martyr

MTAKATIFU WA MTAANI

    (ambaye kwamba Sikukuu yake imeamriwa Kawaida ya Mtakatifu)

Sikukuu iliyo kubwa, ina Oktavo.

(Masomo 314J, 322A, 315J, yaweza kufaa.)

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Msifuni Bwana, enyi wateule wake; Ziadhimisheni Sikukuu zake zenye furaha.
    ZABURI. Sehemu C. (Sikukuu tu).
    WIMBO uliohusika.
    SALA iliyohusika.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Nikaona mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, Watu wa kila taifa, wamesimama mbele ya kiti.
    WIMBO uliohusika.

Sala ya Adhuhuri

Kama kawaida ya Mtakatifu.


 

A Saint of this country (?)

KAWAIDA YA MALAIKA

ZABURI na Antifona za kawaida.
WIMBO uliohusika.
SALA iliyohusika.

Sala ya Adhuhuri

    SOMO. Nalisikia sauti ya Malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi, na elfu mara elfu, wakisema kwa sauti kuu, Wokovu una Mungu wetu.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Mbele ya Malaika nitakuimbia zaburi.
    R. Mbele ya Malaika nitakuimbia zaburi.
    V. Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu.
    R. Nitakuimbia zaburi.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Mbele ya Malaika nitakuimbia zaburi.
    V. Enyi Malaika zote.
    R. Msujuduni Mungu.

Sala ya Ukumbusho

    Ant. Hawa wote ni roho waabuduo, Wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu.
    V. Malaika alisimama mbele ya madhabahu.
    R. Mwenye chetezo cha dhahabu mkononi mwake.

Common of an Angel

 

Return to the Zanzibar Prayer Book

Web author: Charles Wohlers U. S. EnglandScotlandIrelandWalesCanadaWorld