The Book of Common Prayer
United States England Scotland Ireland Wales Canada World

    Kitabu cha Sala za Kanuni (1918)
The Zanzibar Book of Common Prayer in Swahili

 

SEHEMU

ZA

SALA

ZINAZOBADILIKA
 


 

Prayers for the Christian Year

MAJILIO

ZABURI na Antifona za kawaida.
Asubuhi: WIMBO 15.
Jioni: WIMBO 16.
SALA iliyohusika.

Sala ya Adhuhuri

SOMO. Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi, na tuyavue matendo ya giza, na kuzi vaa silaha za nuru.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Ee BWANA, utuonyeshe rehema zako.
    R. Ee BWANA, utuonyeshe rehema zako.
    V. Utupe wokovu wako.
    R. Rehema zako.
    V. Atukuzwe, etc.
   
R. Ee BWANA, utuonyeshe rehema zako.
    V. Ee BWANA, utukumbuke kwa kibali.
    R. Utujilie kwa wokovu wako.

Siku za kazi wote wapige magoti, na Mhudumu aseme,

Bwana, uturehemu.
    Kristo, uturehemu.
Bwana, uturehemu.

Baba yetu (kimoyomoyo).
V. Usitutie majaribuni.
R. Lakini utuokoe na yule mwovu.
V. Ee BWANA, Mungu wa majeshi, uturudishe.
R. Uangazishe uso wako nasi tutaokoka.
V. Ee Kristo, uondoke, uwe msaada wetu.
R. Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.
V. Ee BWANA, usikie kuomba kwetu.
R. Kilio chetu kikufikie.

Ndipo Mhudumu asimame, aimalize sala kama kawaida.

Sala ya Ukumbusho wa Majilio

    Ant. Njoo, Ee Bwana, utujie kwa amani, Ili tufurahi mbele zako kwa moyo mkamilifu.
    V. Uje, utufanye huru.
    R. Ee BWANA, Mungu wa majeshi.

Sala ya S. B. ya Majilio iliyotangulia
 

Advent

Translations of some common words:

  Zab., Zaburi: Psalm(s)
  Wimbo: Hymn
  Sala: Prayer or Collect
  Sala ya Asubuhi: Morning Prayer
  Sala ya Adhuhuri: Noontime Prayer
  Sala ya Jioni: Evening Prayer
  Sala ya Usiku: Night Prayer or Compline
  Sala ya Ukumbusho wa ...: Memorial Prayer of ...
  Bwana: Lord
  Somo: Lesson
  Baba yetu: Our Father (Lord's Prayer)
  S. B.: Siku ya Bwana, Sunday
  Jumatatu: Monday
  Jumanne: Tuesday
  Jumatano: Wednesday
  Alhamisi: Thursday
  Ijumaa: Friday
  Jumamosi: Saturday
  Ant.: Antiphon
 

S. B. I Majilio

Ee Bwana, katika maisha haya yasiyodumu ulikuja kwa unyenyekevu mkuu utuangalie: Tunakusihi uuamshe uweza wako, uje, uyaepushie mbali nasi matendo ya giza, na kutuvika silaha za nuru; ili, siku ya mwisho, utakaporudi kwa utukufu wa enzi yako kuwahukumu wahai na wafu, tufufukie maisha yasiyo na mwisho. Uishiye na kumiliki pamoja na Mungu Baba, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

1 Advent

S. B. II Majilio

Ee Bwana, tunakusihi: Uiamshe mioyo yetu tumfanyizie njia Mwana wako pekee; ili nia zetu zisafishwe kwa kuja kwake, nasi tustahili kukutumikia. Kwa Yeye.
 

2 Advent

S. B. III Majilio

Ee Bwana, tunakusihi: Uyatege masikio yako kwa sala zetu; uje, utuangalie, ili nuru yako iziangaze nia zetu za giza. Uishiye na kumiliki pamoja na Mungu Baba, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

3 Advent

Robo Mwaka

Jumatano

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Utujalie tuitazamie kwa furaha Sikukuu ya ukombozi wetu; ili kwa msaada wako tuokoke katika maisha haya, na kwa ukarimu wako tupewe thawabu ya furaha za milele. Kwa.

Ijumaa

Ee Bwana, tunakuomba: Uje na uweza wako; utujalie tuzidi kulitumainia pendo lako, na kuwekwa huru katika mabaya yote. Uishiye na kumiliki pamoja na Mungu Baba, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Jumamosi

Ee Mungu, unaona ya kuwa tunateswa sana kwa sababu ya upotofu wetu: Utujalie, tunakusihi; tufarijiwe kwa kuja kwako. Uishiye na kumiliki pamoja na Mungu Baba, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

Ember Days

S. B. IV Majilio

Ee Bwana, tunakusihi: Uuamshe uweza wako, uje, utusaidie kwa nguvu nyingi; utupe msaada wa neema yako, ili rehema zako zitusafishie njia yetu tuliyoiziba kwa dhambi zetu. Uishiye na kumiliki pamoja na Mungu Baba, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

4 Advent

Des. 24. Mkesha wa Kuzaliwa.
    Mwenyezi Mungu, watujalia kila mwaka furaha ya kuitazamia Sikukuu ya wokovu wetu: Utujalie sisi tuliomkubali Mwana wako pekee kuwa Mwokozi wetu; tusimame mbele zake bila hofu ajapo kuhukumu. Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

Christmas Vigil

KUZALIWA KWA BWANA

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Mfalme wa amani ametukuzwa Kuliko wafalme wote wa dunia. Haleluya.
    ZABURI Sehemu A. (Kila siku ya Oktavo).
    WIMBO 17.

Sala

Mwenyezi Mungu, ulitupa Mwana wako pekee autwae utu wetu, na, kama majira haya, kuzaliwa na Bikira safi: Utuialie sisi tuliozaliwa mara ya pili na kufanyika watoto wako kwa kuchaguliwa na kwa neema; tufanywe upya kila siku kwa Roho wako Mtakatifu. Kwa Yeye, Bwana wetu Yesu Kristo Mwana wako; Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Mara walikuwapo pamoja na huyo Malaika wingi wa jeshi la mbinguni, Wakimsifu Mungu. Haleluya.
    WIMBO 18.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Ee Yesu, Mwana wa Bikira,
    Twakutolea sifa zetu,
Pamoja naye Mungu Baba,
    Na Mungu Roho Mtakatifu.   Amin.

SOMO. Wewe, BWANA, hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi, na mbingu ni kazi za mikono yako.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Neno alifanyika mwili. Haleluya. Haleluya.
    R. Neno alifanyika mwili. Haleluya. Haleluya.
    V. Akakaa kwetu.
    R. Haleluya. Haleluya.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Neno alifanyika mwili. Haleluya. Haleluya.
    V. Yeye ataniita. Haleluya.
    R . Wewe Baba yangu. Haleluya.

Sala ya Ukumbusho wa Kuzaliwa

    Ant. Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Haleluya.
    V. BWANA ameufunua. Haleluya.
    R. Wokovu wake. Haleluya.
 

Christmas Day

Des. 26. Stefano, Sh. wa Kwanza.   2.   (na Jan. 2)
WIMBO 19.

Sala

Mwenyezi Mungu, wa milele, ulitabaruku malimbuko ya Mashahidi wako katika damu ya Stefano Mbarikiwa: Utujalie, tunakusihi; atuwie mwombezi wetu, kama vile alivyowaombea adui zake. Kwa.
 

St. Stephen

Des. 27. Yohana, Mtume, Mtunga Injili.   2.   (na Jan. 3)
WIMBO 20.

Sala

Ee Bwana, mwenye rehema, tunakusihi, uliangaze Kanisa lako kwa fadhili zako: Ili litiwe nuru kwa mafundisho ya Yohana Mbarikiwa, Mtume wako na Mtunga Injili; na kuzidi kwenda katika nuru ya kweli yako, hatimaye likapate kuifikia nuru ya maisha ya milele. Kwa.
 

St. John the Evangelist

Des. 28. Wasio na Hatia.   2.   (na Jan. 4)
WIMBO 21.

Sala

Mwenyezi Mungu, ulikamilisha sifa kwa vinywa vya watoto nao wanyonyao, ukapenda watoto wadogo wakutukuze kwa kufa wala si kwa kunena: Uyafishe ndani yetu mabaya yote, na kutufanya imara kwa neema yako; ili tulitukuze Jina lako takatifu sikuzote kwa maisha safi, na kwa imani iliyo thabiti hata kufa. Kwa.
 

Holy Innocents

Des.29. Tomaso wa Canterbury, A. Sh. 3
WIMBO 19.

Sala

Ee Mungu, kwa ajili ya Kanisa lako Tomasa wa Canterbury, Askofu Mtukufu, aliuawa kwa panga za watu wakorofi: Tunakusihi; wote wajitakiao msaada kwake wapate kuombewa naye, na kwa rehema zako uwajalie wokovu. Kwa.
 

Thomas of Canterbury

S. B. Baada ya Kuzaliwa

Mwenyezi Mungu, wa milele, tunakuomba: Utuongoze siku zote kwa mapenzi yako mema; ili tustahili kulichukua Jina la Mwana wako Mpendwa, na kumtendea yaliyo mazuri. Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

Sunday after Christmas

Des. 31. Silvesta, A. Mu. 3
WIMBO 51.

Sala

Ee Mungu wa wokovu wetu, ulimweka Silvesta Mtakatifu awe Askofu na Kuhani Mkuu katika Kanisa lako, ukampa amani mbele ya adui zake: Utujalie, tunakusihi, amani yako siku zetu zote; ili tuzidi kuendelea katika njia ya wokovu, na kuifurahia maisha ya utulivu. Kwa.
 

 
Sylvester

Jan. 1. Kutahiriwa kwa Bwana.   2

Mwenyezi Mungu, ulipenda Mwana wako Mtukufu atahiriwe, aifuate torati kwa ajili ya wanadamu: Utujalie kutahiriwa kwa kweli, kwa rohoni; ili, tamaa za dunia na za mwili zikifishwa ndani yetu, tuyatii mapenzi yako katika mambo yote. Kwa Yeye.

Baada ya Jan. 1 zitumike Zaburi na Antifona za kawaida.

Ikiwa Jan. 2, 3, 4, au 5 ni S.B. ibada yake ndiyo ya Jina Takatifu, Yesu. (taz. Aug. 7.)
 

 
Circumcision

Jan. 5. Mkesha wa Ufunuo

Kama S. B. baada ya Kuzaliwa
 

Vigil of Epiphany

UFUNUO WA BWANA

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Nuru utokaye Nuru, umeonekana, Ee Kristo; Kwako Mamajusi walileta tunu. Haleluya.
    ZABURI Sehemu A. (Sikukuu, na S. B.).
    WIMBO 22.

Sala

Ee Mungu, uliwafunulia mataifa Mwana wako pekee kwa kutokea nyota: Kwa rehema zako utubariki sisi tunaokujua sasa kwa imani; ili baada ya maisha haya tuufurahie Uungu wako Mtukufu. Kwa Yeye.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Mamajusi walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno; Wakaingia nyumbani wakamwona mtoto. Haleluya.
    WIMBO 23.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Kwa Ufunuo wako, Bwana,
    Twakuhimidi sana leo,
Pamoja naye Mungu Baba,
    Na Mungu Roho Mtakatifu. Amin.

SOMO. Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, na utukufu wa BWANA umekuzukia.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Wote watakuja kutoka Sheba. Haleluya. Haleluya.
    R. Wote watakuja kutoka Sheba. Haleluya. Haleluya.
    V. Wataleta dhahabu na uvumba.
    R. Haleluya. Haleluya.
    V. Atukuzwe. etc.
    R. Wote watakuja kutoka Sheha. Haleluya. Haleluya.
    V. Mwabuduni BWANA. Haleluya.
    R. Kwa uzuri wa utakatifu. Haleluya.

Sala ya Ukumbusho wa Ufunuo

    Ant. Twafanya Sikukuu yenye kupambwa miujiza mitatu; Leo nyota iliwaongoza Mamajusi kwenve zizi, leo maji yaligeuka kuwa divai arusini, leo Kristo alikubali kubatizwa na Yohana katika Yordani, ili atuokoe. Haleluya.
    V. Wote watakuja kutoka Sheba. Haleluya.
    R. Wataleta dhahabu na uvumba. Haleluya.
 

Epiphany

S. B. I Ufunuo

Ee Bwana, tunakusihi: Ufikilize kwa wema wako wa mbinguni haja za watu wakuombao; ili wajue yawapasayo kuyatenda, na kupewa nguvu ya kuyatimiza wayajuayo. Kwa.
 

1 Epiphany

S. 8. Ufunuo

Ee Mungu, ulipenda Mwana wako wa azali aonekane amejitwalia ubinadamu wetu: Utujalie; kama vile alivyo-kubali kufanana nasi kwa mambo yote ya mwilini, sisi nasi tufananishwe naye kwa mambo yote ya moyoni. Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Baada ya Siku ya Nane ya Ufunuo hata Kwaresima Ibada ndiyo ya kawaida, isipokuwa ni Sikukuu.
 

Octave of Epiphany (?)

S. B. II Ufunuo

Mwenyezi Mungu wa milele, unayatawala yaliyo mbinguni na yaliyo duniani: Uzisikie kwa rehema dua za watu wako; na kutujalia amani siku zetu zote. Kwa.
 

2 Epiphany

S. B. III Ufunuo

Mwenyezi Mungu wa milele, uutazame kwa huruma udhaifu wetu: Uunyoshe mkono wako wa kuume; na kutuhifadhi katika hatari na shida zetu zote. Kwa.
 

3 Epiphany

S. B. IV Ufunuo

Ee Mungu, unajua ya kuwa sisi tumo hatarini sana, wala hatuwezi kusimama kwa sababu ya udhaifu wa ubinadamu: Utujalie uzima wa roho na wa mwili; ili, kwa' msaada wako, tusishindwe na mambo yatupatayo kwa ajili ya dhambi zetu. Kwa.
 

4 Epiphany

S. B. V Ufunuo

Ee Bwana, tunakusihi: Uwalinde watu wako kwa pendo lisilokwisha; ili tukilitegemea tumaini la neema yako ya mbinguni, tuhifadhiwe kwa himaya yako ya daima. Kwa.
 

5 Epiphany

S. B. VI Ufunuo

Ee Mungu, Mwana wako Mtakatifu alitokea makusudi azivunje kazi za Shetani, na kutufanya wana wa Mungu: Tunakusihi, utujalie sisi tulio nalo tumaini hili, tuwe watakatifu kama Yeye alivyo mtakatifu; ili, atakapotokea tena, tufananishwe naye katika ufalme wako mtukufu wa milele. Kwa Yeye.
 

6 Epiphany

SEPTUAJESIMA

Yote kama kawaida isipokuwa haya,

Katika Sala ya Jioni ya kwanza ya Septuajesima V na R ya mwisho huimbwa, au kusemwa, hivi.

    V. Tumhimidi BWANA. Haleluya. Haleluya.
    R. Tumshukuru Mungu. Haleluya. Haleluya.
    Na tokea wakati huu imekatazwa neno hili Haleluya lisiimbwe, wala kusemwa, katika antifona, wala katika nyimbo, wala po pote hata Pasaka.

S. B. Septuajesima

Ee Bwana, tunakusihi: Uzisikilize kwa upole sala za watu wako; ili sisi, tunaoteswa kwa haki kwa sababu ya dhambi zetu, tupate kwa rehema zako kuachiliwa, kwa ajili ya utukufu wa Jina lako. Kwa.
 

Septuagesima

S. B. Seksajesima

Ee Mungu, unaona ya kuwa sisi hatutumainii tendo letu liwalo lote: Kwa neema yako, ukubali kutulinda; ili tuhifadhiwe na mabaya yote. Kwa.
 

Sexagesima

S. B. Kwinkwajesima

Ee Bwana, umetufundisha ya kuwa matendo yetu yote pasipo upendo hayafai: Tunakusihi; utumiminie mioyoni mwetu upendo huo, na kwa rehema zako utujalie kuzidi kuzitubia dhambi zetu. Kwa.
 

Quinquagesima

Jumatano ya Majivu

Mwenyezi Mungu wa milele, huchukii kitu cho chote ulichokifanya, bali waziondoa dhambi za wote waliotubu: Utuumbie moyo mpya na uliopondeka; ili tujililie dhambi zetu kama itupasavyo, na kusamehewa nawe kabisa, Ee Mungu mwenye rehema nyingi. Kwa.

Alhamisi

Ee Mungu, wachukizwa kwa kosa na kuridhishwa kwa toba: Uzikubali kwa rehema sala za watu wako wakuombao; uiepushie mbali nasi hasira yako tunayoistahili kwa dhambi zetu. Kwa.

Ijumaa

Ee Bwana, tunakusihi: Utusaidie kwa hisani yako katika mfungo wetu tuliouanza ; ili tupate kufanya bidii katika mioyo yetu, kama vile tunavyoionyesha miilini mwetu. Kwa.

Jumamosi

Ee Bwana, uyafanikishe maombi yetu: Utujalie tuufululize vema mfungo huu; ulio amriwa kwa afya yetu ya mwili na ya roho. Kwa.
 

Ash Wednesday

KWARESIMA

(Tokea S. B. ya 1 Kwaresima)

ZABURI na Antifona za kawaida.
Asubuhi: WIMBO 24.
Jioni: WIMBO 25.
SALA iliyohusika.

Sala ya Aduhuri

SOMO. Tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa. Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Kwa manyoya yake atakufunika.
    R. Kwa manyoya yake atakufunika.
    V. Chini ya mbawa zake utapata kimbilio.
    R. Atakufunika.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Kwa manyoya yake atakufunika.
    V. Uaminifu wake ni ngao na kigao.
    R. Hutaogopa hofu ya usiku.

Siku za kazi wote wapige magoti, na Mhudumu aseme,

Bwana, uturehemu.
    Kristo, uturehemu.
Bwana, uturehemu.

Baba yetu (kimoyomoyo).
V. Usitutie majaribuni.
R. Lakini utuokoe na yule mwovu.
V. Ee BWANA, Mungu wa majeshi, uturudishe.
R. Uangazishe uso wako nasi tutaokoka.
V. Ee Kristo, uondoke, uwe msaada wetu.
R. Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.
V. Ee BWANA, usikie kuomba kwetu.
R. Kilio chetu kikufikie.

Ndipo Mhudumu asimame, aimalize sala kama kawaida.

Sala ya Ukumbusho wa Kwaresima

    Ant. Ee Mungu, unirehemu sawasawa - na fadhili zako; Kiasi cha wingi wa rehema zako uyafute makosa yangu.
    V. Uzifute hatia zangu zote.
    R. Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.

Sala ya siku ya kazi ya Kwaresima.
 

Lent

(Until the first Sunday in Lent)

S. B. I Kwaresima

Ee Bwana, ulifunga kwa ajili yetu siku arobaini mchana na usiku: Utujalie tufunge chakula hata mwili utiishwe kwa roho; ili tufuate sikuzote maelekezo yako katika haki na utakatifu halisi, kwa heshima na utukufu wako. Uishiye na kumiliki pamoja na Mungu Baba, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Jumatatu

Ururudishe, Ee Mungu wa wokovu wetu: Uielemishe mioyo yetu kwa malezi yako ya mbinguni; ili tufaidiwe kwa kufunga kwetu wakati huu wa Kwaresima. Kwa.

Jumanne

Ee Bwana, uiangalie jamaa hii ya watu wako: Utujalie sisi tujirudi kwa kuzifisha tamaa za mwili; ili mbele zako mioyo yetu iangazwe kwa kukuonea shauku. Kwa.

Jumatano, Robo Mwaka

Ee Bwana, tunakusihi: Kwa huruma zako uzisikilize dua zetu; uunyoshe mkono wako wa kuume, na kutuondolea mambo yote yanayotupinga, Kwa.

Alhamisi

Ee Bwana, tunakuomba, uikubali nia njema ya watu wako: Ili tupate kujiweza mwili kwa kufunga; na kuburudika moyoni kwa mazao ya matendo mema. Kwa.

Ijumaa, Robo Mwaka

Ee Bwana, utuonee huruma sisi watumishi wako: Tuzidi kujiweka kwako kwa neema yako; ili turehemiwe na kufarijiwa kwa ukarimu wako. Kwa.

Jumamosi, Robo Mwaka

Ee Bwana, tunakusihi: Uwaangalie watu wako kwa upendo wako; na kwa rehema zako uyageuzie mbali nasi mapigo ya hasira yako. Kwa.
 

1 Lent

(Robo Mwaka = Ember Days)

S. B. II Kwaresima

Mwenyezi Mungu, unaona ya kuwa sisi hatuna wema wo wote: Utulinde ndani na nje; ili tuhifadhiwe na madhara yote yawezayo kuupata mwili, na kusafishwa na mawazo mabaya ya moyoni. Kwa.

Jumatatu

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Uwajalie watoto wako wafunge chakula kwa kujinyima mwilini; na kujiepusha na dhambi kwa kuifuata haki. Kwa.

Jumanne

Ee Bwana, tunakuomba, uikamilishe ndani yetu kazi hii ya kufunga: Ili kwa maagizo yako tuyajue yatupasayo; na kwa uweza wako tuyatimize. Kwa.

Jumatano

Ee Bwana, tunakusihi, uwatazame kwa rehema watu wako: Utujalie tuyaepuke mabaya yote; kama vile ulivyotuagiza kujihinisha chakula. Kwa.

Alhamisi

Ee Bwana, tunakusihi, utupe msaada wa neema yako: Ili tujitahidi katika kufunga na kusali; na kuokolewa na adui zetu zote za mwili na za roho. Kwa.

Ijumaa

Mwenyezi Mungu, tunakuomba, utujalie neema yako: Ili tutakaswe kwa kufunga kwetu; na kwa mioyo safi tuikaribie Sikukuu inayokuja. Kwa.

Jumamosi

Ee Bwana, tunakusihi, utujalie tufunge kwa faida ya roho zetu: Ili tuongezewe nguvu za rohoni; kwa ajili ya kujirudi miilini mwetu. Kwa.
 

2 Lent

S. B. III Kwaresima

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Uzitafakari haja za watu wako wanyenyekevu; uunyoshe mkono wako wa kuume ili utuhifadhi na adui zetu zote. Kwa.

Jumatatu

Ee Bwana, tunakuomba: Kwa rehema zako utumiminie mioyoni mwetu neema yako; Ili tunavyopunguza chakula chetu, vivyo hivyo tujiepushe na upotovu wote unaotudhuru. Kwa.

Jumanne

Mwenyezi Mungu, mwenye rehema: Utusikie kwa kibali; na kwa wema wako utupe kipawa chako cha uzuilifu wa tamaa. Kwa.

Jumatano

Ee Bwana, tunakusihi: Utujalie kuelimishwa kwa kufunga na kwa kuepuka mabaya; ili tuzidi kupata kwa wingi fadhili zako. Kwa.

Alhamisi

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Utujalie tusafishwe kwa kufunga kwetu; na kupata kibali machoni pako. Kwa.

Ijumaa

Ee Bwana, tunakuomba, kwa wema wako uukubali mfungo wetu: Ili kama tunavyojinyima chakula cha mwilini; vivyo hivyo tujihadhari na maovu ya moyoni. Kwa.

Jumamosi

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Uwajalie wao wautiishao mwili kwa kufunga chakula; wajitenge na dhambi kwa kuifuatisha haki. Kwa.
 

3 Lent

S. B. IV Kwaresima

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Utujalie neema yako; ili tusizidi kuteswa kwa ubaya wa matendo yetu, bali tuburudishwe kwa faraja ya neema yako. Kwa.

Jumatatu

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Utujalie sisi tunaozishika nyakati hizi za kufunga kila mwaka; tukupendeze kwa mwili na roho. Kwa.

Jumanne

Ee Bwana, tunakuomba: Kwa kufunga kwetu tuzidi kuutengeneza mwenendo wetu; na kujipatia daima msaada wa fadhili zako. Kwa.

Jumatano

Ee Mungu, unawapa wenye haki thawabu na wenye dhambi masamaha kwa njia ya kufunga: Uturehemu sisi tukuombao; ili kwa kuungama dhambi tujiweke tayari kupokea ghofira. Kwa.

Alhamisi

Mwenyezi Mungu, tunakuomba: Utujalie sisi tunao-adhibiwa kwa kufunga tufurahishwe kwa ibada yetu; ili tupunguziwe tamaa za duniani, na kuzidi kuambatana na mambo ya mbinguni. Kwa.

Ijumaa

Ee Mungu, unafanya upya ulimwengu kwa Sakramenti za ajabu: Utujalie, tunakusihi; Kanisa lako lifaidiwe kwa ibada za milele, wala lisikose msaada wako hapa duniani. Kwa.

Jumamosi

Ee Bwana, tunakusihi: Ibada yetu ya upendo iwe na mazao tele kwa neema yako; kwa maana kufunga kwetu kwafaa tupatapo kibali kwa rehema zako. Kwa.
 

4 Lent

WAKATI WA MATESO

ZABURI na Antifona za kawaida.
Asubuhi: WIMBO 26.
Jioni: WIMBO 27.
SALA iliyohusika.

Sala ya Adhuhuri

SOMO. Damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Kinywani mwa simba uniokoe, Ee BWANA.
    R. Kinywani mwa simba uniokoe, Ee BWANA.
    V. Naam, toka pembe za nyati umenijibu.
    R. Uniokoe, Ee BWANA.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Kinywani mwa simba uniokoe, Ee BWANA.
    V. Usiniondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji.
    R. Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu.

Siku za kazi wote wapige magoti, na Mhudumu aseme,

Bwana, uturehemu.
    Kristo uturehemu.
Bwana, uturehemu.

Baba yetu (kimoyomoyo).
V. Usitutie majaribuni.
R. Lakini utuokoe na yule mwovu.
V. Ee BWANA, Mungu wa majeshi, uturudishe.
R. Uangazishe uso wako nasi tutaokoka.
V. Ee Kristo, uondoke, uwe msaada wetu.
R. Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.
V. Ee BWANA, usikie kuomba kwetu.
R. Kilio chetu kikufikie.

Ndipo Mhudumu asimame, aimalize sala kama kawaida.
 

Season of the Passion

S. B. ya Mateso

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Uiangalie kwa neema jamaa ya watu wako; ili kwa ukarimu wako miili yao itawaliwe, na roho zao zitunzwe. Kwa.

Jumatatu

Ee Bwana, tunakusihi: Uutakase mfungo wetu; na kwa rehema zako utusamehe makosa yetu. Kwa.

Jumanne

Ee Bwana, tunakuomba, utukubali tufungapo: Ili tuistahili neema yako kwa fidia hii ya dhambi zetu; hata na tuletewe dawa ya milele. Kwa.

Jumatano

Ee Mungu, uiangaze mioyo yao wenye imani kwa kuutakasa mfungo huu: Uwajalie moyo wa ibada; ili uwasikilize kwa kibali wakuombapo. Kwa.

Alhamisi

Mwenyezi Mungu, tunakuomba: Utujalie kurudishiwa heshima ya ubinadamu kwa kujinyima kwetu; kwa maana imeharibika kwa kujipendeza kwetu. Kwa.

Ijumaa

Ee Bwana, tunakusihi, utupe kwa ukarimu neema yako: Ili tukomeshe dhambi kwa kuhiari maadili; na kwa kurudiwa sasa tuiepuke adhabu ya milele. Kwa.

Jumamosi

Ee Bwana, tunakuomba, watu wako wazidi kukuabudu: Ili wafundishwe kwa ibada takatifu; na kama vile walivyo-pokea kibali kwako, wazidi kukutolea sadaka. Kwa.
 

Passion Sunday

S. B. ya Mitende

Mwenyezi Mungu wa milele, ulimtuma Mwokozi wetu autwae mwili wetu na kuu vumilia msalaba, ili tuufuatishe unyenyekevu wake: Utujalie tuyakumbuke mateso yake itupasavyo; ili, kwa njia ya saburi yake, tuufikie utukufu wa kufufuka kwake. Kwa Yeye.
 

Palm Sunday

Jumatatu katika Juma Takatifu

Mwenyezi Mungu, upende kutusikiliza: Utuburudishe kwa ajili ya Mateso ya Mwana wako pekee; kwa maana tumedhoofika kwa mabaya mengi yaliyotupata. Kwa Yeye.

Jumanne katika Juma Takatifu

Mwenyezi Mungu, wa milele, tunakuomba, uzikubali dua zetu: Utujalie tuufululize ukumbusho wa Mateso ya Bwana wetu; ili tustahili kupewa masamaha aliyotupatia. Kwa Yeye.

Jumatano katika Juma Takatifu

Ee Mungu, ulipenda Mwana wako auvumilie msalaba, ili aziepushie mbali nasi nguvu za Shetani: Utujalie, tunakuomba; sisi watumishi wako tuipate neema ya kufufuliwa. Kwa Yeye.
 

Monday in Holy Week

ALHAMISI YA AMRI

Atukuzwe isisemwe kamwe po pote.

Sala ya Asubuhi

Inaanzia Zaburi (zikiisha sala za siri).

    Ant. Mungu hakumwachilia Mwana wake mwenyewe, Bali alimtoa kwa ajili yetu.
    (Isemwe nzima mwanzo na mwisho pia.)

ZAB. 40

1. Nalimngoja BWANA kwa saburi, *
    Akaniinamia akakisikia kilio changu.
2. Akanipandisha toka shimo la uharibifu, *
    Toka udongo wa utelezi.
3. Akaisimamisha miguu yangu mwambani, *
    Akaziimarisha hatua zangu.
4. Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, *
    Ndio sifa zake Mungu wetu.

5. Wengi wataona na kuogopa, *
    Nao watamtumaini BWANA.
6. Yu heri aliyemfanya BWANA kuwa tumaini lake; *
    Wala hakuwaelekea wenye kiburi, wala hao wanao-geukia uongo.
7. BWANA Mungu wangu, umefanya kwa wingi miujiza yako na mawazo yako kwetu; *
    Hakuna awezaye kufananishwa nawe.
8. Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, *
    Ni mengi sana hayahesabiki.
9. Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, masikio yangu umeyazibua, *
    Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka ;

10. Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, katika gombo la chuo nimeandikiwa, *
    Niyafanye mapenzi yako.
11. Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; *
    Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.
12. Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa; *
    Sikuizuia midomo yangu; BWANA, unajua.
13. Sikusitiri haki yako moyoni mwangu; *
    Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.
14. Sikuficha fadhili zako wala kweli yako *
    Katika kusanyiko kubwa.

15. Nawe, BWANA, usinizuilie rehema zako, *
    Fadhili zako na kweli yako zinihifadhi daima,
16. Kwa maana mabaya yasiyohesabika *
    Yamenizunguka mimi.
17. Maovu yangu yamenipata, *
    Wala siwezi kuona,
18. Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu, *
    Na moyo wangu umeniacha.

19. Ee BWANA, uwe radhi kuniokoa, *
    Ee BWANA, unisaidie hima.
20. Waaibike, wafedheheke pamoja, *
    Wanaoitafuta nafsi yangu waiangamize.
21. Warudishwe nyuma, watahayarishwe, *
    Wapendezwao na shari yangu.
22. Wakae hali ya ukiwa na iwe aibu yao, *
    Wanaoniambia, Ewe! Ewe!
23· Washangilie, wakufurahie, *
    Wote wakutafutao.
24. Waupendao wokovu wako *
    Waseme daima, Atukuzwe BWANA.
25. Nami ni maskini na mhitaji, *
    Bwana atanitunza.
26. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, *
    Ee Mungu wangu, usikawie.
    (Isisemwe Atukuzwe.)

    Ant. Mungu hakumwachilia Mwana wake mwenyewe; Bali alimtoa kwa ajili yetu.
    Ant. Kama mwana-kondoo BWANA alipelekwa machinjoni; Naam, hakufumbua kinywa chake

ZAB. 54

1. Ee Mungu, kwa Jina lako uniokoe, *
    Na kwa uweza wako unifanyie hukumu.
2. Ee Mungu, uyasikie maombi yangu, *
    Uyasikilize maneno ya kinywa changu.
3. Kwa maana wageni wamenishambulia; *
    Watu watishao wananitafuta nafsi yangu.
4. Hawakumweka Mungu mbele yao; *
    Tazama, Mungu ndiye anayenisaidia mimi.
5. Bwana ndiye anayenitegemeza nafsi yangu; *
    Atawarudishia adui zangu ubaya wao.
6. Uwaangamize kwa uaminifu wako; *
    Kwa ukunjufu wa moyo nitakutolea dhabihu.
7. BWANA, nitalishukuru Jina lako maana ni jema, *
    Kwa kuwa limeniokoa na kila taabu.
8. Na jicho langu limeridhika *
    Kwa kuwatazama adui zangu.
    (Isisemwe Atukuzzoe.)

    Ant. Kama mwana-kondoo BWANA alipelekwa machinjoni; Naam, hakufumbua kinywa chake.
    Ant. Enyi nyote mpitao, angalieni, Mtazame kama kuna majonzi yo yote mfano wa majonzi yangu.

ZAB. 88

1. Ee BWANA, Mungu wa wokovu wangu, *
    Mchana na usiku nimelia mbele zako.
2. Maombi yangu yafike mbele zako, *
    Uutegee ukelele wangu sikio lako.
3. Maana nafsi yangu imeshiba taabu, *
    Na uhai wangu umekaribia kuzimu.
4. Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; *
    Nimekuwa kama mtu asiye na msaada.
5. Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, *
    Kama waliouawa walalao makaburini.
6. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena *
    Wametengwa mbali na mkono wako.

7. Mimi umenilaza katika shimo la chini, *
    Katika mahali penye giza vilindini.
8. Ghadhabu yako imenilemea; *
    Umenitesa kwa mawimbi yako yote.
9. Wanijuao umewatenga nami, *
    Umenifanya kuwa chukizo kwao.
10. Nimefungwa wala siwezi kutoka; *
    Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso.

11. Ee BWANA, nimekuita kila siku; *
    Nimekunyoshea Wewe mikono yangu.
12. Wafu je! utawafanyia miujiza? *
    Au waliofariki watasimama na kukuhimidi?
13. Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? *
    Au uaminifu wako katika uharibifu?
14. Miujiza yako itajulikana gizani? *
    Au haki yako katika nchi ya usahaulifu ?

15. Lakini mimi nimekulilia Wewe, BWANA, *
    Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia.
16. BWANA, ya nini kuitupa nafsi yangu, *
    Na kunificha uso wako?
17. Nateswa mimi hali ya kufa tangu ujana; *
    Nimevumilia vitisho vyako na kufadhaika.
18. Hasira zako kali zimepita juu yangu; *
    Maogofyo yako yameniangamiza.
19. Yamenizunguka kama maji mchana kutwa; *
    Yamenisonga yote pamoja.
20. Mpenzi na rafiki umewatenga nami, *
    Nao wanijuao wamo gizani.
    (Isisemwe Atukuzwe.)

    Ant. Enyi nyote mpitao, angalieni, Mtazame kama kuna majonzi yo yote mfano wa majonzi yangu.

    WIMBO, V. na R. hapana.
    ANT. BENEDICTUS. Yule mwenye kumsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni.
    (Isemwe nzima mwanzo na mwisho pia.)

Ikiisha BENEDICTUS na Antifona yake mara husemwa na wote, wamepiga magoti,

    Kristo alikuwa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
    Baba yetu (kimoyomoyo).

ZAB. 51

    (Isemwe na wote pamoja kwa sauti ndogo.)
1. Ee Mungu, unirehemu, *
    Sawasawa na fadhili zako.
2. Kiasi cha wingi wa rehema zako *
    Uyafute makosa yangu.
3. Unioshe kabisa na uovu wangu; *
    Unitakase dhambi zangu.
4. Maana nimejua mimi makosa yangu, *
    Na dhambi yangu i mbele yangu daima.
5. Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, *
    Na kufanya maovu mbele za macho yako.
6. Wewe ujulike kuwa una haki unenapo, *
    Na kuwa safi utoapo hukumu.
7. Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; *
    Mama yangu alinichukua mimba hatiani.
8. Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni; *
    Nawe utanijulisha hekima kwa siri.
9. Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi; *
    Unioshe nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
10. Unisikize furaha na shangwe, *
    Mifupa uliyoiponda ifurahi.
11. Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; *
    Uzifute hatia zangu zote.
12. Ee Mungu, uniumbie moyo safi; *
    Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.
13. Usinitenge na uso wako; *
    Wala Roho wako Mtakatifu usiniondolee.
14. Unirudishie furaha ya wokovu wako; *
    Unitegemeze kwa roho ya wepesi.
15. Nitawafundisha wakosaji njia zako, *
    Na wenye dhambi watarejea kwako.
16. Ee MUNGU, Mungu wa wokovu wangu, uniponye na damu za watu, *
    Na ulimi wangu utaiimba haki yako.
17. Ee Bwana, uifumbue midomo yangu, *
    Na kinywa changu kitazinena sifa zako.
18. Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa; *
    Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
19. Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; *
    Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.
20. Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako; *
    Uzijenge kuta za Yerusalemu.
21. Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki, *
    Na sadaka za kuteketezwa na kafara.
22. Ndipo watakapotoa ng'ombe *
    Juu ya madhabahu yako.
    (Isisemwe Atukuzwe.)

Ndipo hufuata pasipo BWANA akae nanyi wala Tuombe,

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Uiangalie jamaa hii ya
watu wako; ambayo kwa ajili yake Bwana wetu Yesu Kristo hakukataa kutiwa mikononi mwao wenye madhara, na kuyavumilia maumivu ya msalaba. (Akaseme kimoyomoyo) Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Wala wasiongeze neno.

Sala ya Adhuhuri

Inaanzia Zaburi (zikiisha sala za siri).

ANT. ZAB. hapana.
ZABURI za kawaida.

Zikiisha Zaburi wapige magoti, waseme yote tangu Kristo alikuwa mtii hata mwisho wa sala, kama sala ya asubuhi.

Sala ya Jioni

Imekatazwa isiimbwe.
Inaanzia Zaburi (zikiisha sala za siri).

    Ant. Nitakipokea kikombe cha wokovu; Na kulitangaza Jina la BWANA.
    (Isemwe nzima mwanzo na mwisho pia.)

ZAB. 69

1 Ee, Mungu, uniokoe, *
    Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu.
2. Ninazama katika matope mengi, *
    Pasipowezekana kusimama.
3. Nimefika penye maji ya vilindi, *
    Mkondo wa maji unanigharikisha. •
4. Nimechoka kwa kulia kwangu, *
    Koo yangu imekauka.
5. Macho yangu yamedhoofu *
    Kwa kumngoja Mungu wangu.
6. Wanaonichukia bure ni wengi *
    Kuliko nywele za kichwa changu.
7. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, *
    Adui zangu kwa sababu isiyo kweli.
8. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu *
    Vitu nisivyovichukua.

9. Wewe, Mungu, unajua upumbavu wangu, *
    Wala hukufichwa dhambi yangu.
10. Wanaokungoja Wewe wasiaibishwe, *
    Kwa ajili yangu, Bwana MUNGU wa majeshi.
11. Wanaokutafuta Wewe wasifedheheshwe, *
    Kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli.
12. Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, *
    Fedheha imenifunika uso wangu.
13. Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, *
    Na msikwao kwa wana wa mama yangu.
14. Maana wivu wa nyumba yako umenila, *
    Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.
15. Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, *
    Ikawa laumu juu yangu.
16. Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, *
    Nikawa mithali kwao.

17. Waketio langoni hunisema, *
    Na nyimbo za walevi hunidhihaki.
18. Nami maombi yangu nakuomba Wewe, BWANA, *
    Wakati ukupendezao, Ee Mungu.
19. Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, *
    Katika kweli ya wokovu wako.
20. Uniponye kwa kunitoa matopeni, *
    Wala usiniache nikazama.
21. Na niponywe nao wanaonichukia, *
    Na katika vilindi vya maji.
22. Mkondo usinigharikishe wala vilindi visinimeze, *
    Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu

23. Ee BWANA, unijibu maana fadhili zako ni njema, *
    Kwa kadiri ya rehema zako unielekee.
24. Wala usinifiche uso wako mimi mtumishi wako, *
    Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi.
25. Unikaribie uikomboe nafsi yangu, *
    Kwa sababu ya adui zangu unifidie.
26. Wewe umejua kulaumiwa kwangu, *
    Na kuaibika na kufedheheka kwangu.
27. Mbele zako Wewe wako watesi wangu wote; *
    Laumu imenivunja moyo nami ninaugua sana,
28. Nikangoja aje wa kunihurumia wala hakuna, *
    Na wa kunifariji wala sikumwona mtu.

29. Wakanipa uchungu kuwa chakula changu; *
    Nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki,
30. Meza yao mbele yao na iwe mtego; *
    Naam, wakiwa salama na iwe shabuka.
31. Macho yao yatiwe giza wasione, *
    Na viuno vyao uvitetemeshe daima,
32. Uimwage ghadhabu yako juu yao, *
    Na ukali wa hasira yako uwapate.
33. Matuo yao na yawe ukiwa, *
    Pasiwe na mtu wa kukaa hemani mwao.
34, Maana wanamwudhi mtu uliyempiga Wewe, *
    Wanasimu1ia maumivu yao uliowatia jeraha.
35. Uwaongezee uovu juu ya uovu, *
    Wala wasiingie katika haki yako.
36. Na wafutwe katika chuo cha uhai, *
    Wala pamoja na wenye haki wasiandikwe.

37. Nami niliye maskini na mtu wa huzuni, *
    Mungu, wokovu wako utaniinua.
38. Nitalisifu Jina la Mungu kwa wimbo, *
    Nami nitamtukuza kwa shukrani.
39. Hayo yatampendeza BWANA kuliko ng'ombe, *
    Au ndama mwenye pembe na kwato.
40. Walioonewa watakapoona watafurahi; *
    Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe.
41. Kwa kuwa BWANA huwa sikia wahitaji, *
    Wala hawadharau wafungwa wake.
42. Mbingu na nchi zitamsifu, *
    Bahari na vyote viendavyo ndani yake.
43. Mungu ataiokoa Sayuni na kuijenga miji ya Yuda, *
    Na watu watakaa ndani yake na kuimiliki.
44. Wazao wa watumishi wake watairithi, *
    Nao walipendao Jina lake watakaa humo.
    (Isisemwe Atukuzwe.)

    Ant. Nitakipokea kikombe cha wokovu; Na kulitangaza Jina la BWANA.
    Ant. Nalitazama mkono wangu wa kuume, nikaona, Ya kuwa hakuna mtu anijuaye.

ZAB. 90

1. Wewe, Bwana, umekuwa makao yetu, *
    Kizazi baada ya kizazi.
2. Kabla haijazaliwa milima usijeiumba dunia, *
    Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu.
3. Wamrudisha mtu mavumbini, *
    Usemapo, Rudini, enyi wanadamu.
4. Maana miaka elfu machoni pako *
    Ni kama jana ikiisha kupita na kesha la usiku.

5. Wawagharikisha, huwa kama usingizi, *
    Huwa kama majani yameayo asubuhi.
6. Asubuhi yachipuka na kumea, *
    Jioni yakatika na kukauka.
7. Maana tumetoweshwa kwa hasira yako, *
    Na kwa ghadhabu yako tumefadhaishwa.
8. Umeyaweka maovu yetu mbele zako, *
    Siri zetu katika mwanga wa uso wako.
9. Maana siku zetu zote zimepita katika hasira yako, *
    Tumetowesha miaka yetu kama kite.

10. Siku za miaka yetu ni miaka sabini, *
    Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini;
11. Na kiburi chake ni taabu na ubatili, *
    Maana chapita upesi tukatokomea mara.
12. Ni nani aujuaye uweza wa hasira yako, *
    Na ghadhabu yako kama ipasavyo kicho chako?
13. Basi utujulishe kuzihesabu siku zetu, *
    Tujipatie moyo wa hekima.
14. Ee BWANA, urudi, hata lini? *
    Uwahurumie watumishi wako.

15. Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako, *
    Nasi tutashangilia na kufurahi siku zetu zote.
16. Utufurahishe kwa kadiri ya siku ulizotutesa, *
    Kama miaka ile tuliyoona mabaya.
17. Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako, *
    Na adhama yako kwa watoto wao.
18. Na uzuri wa BWANA Mungu wetu uwe juu yetu, *
    Na kazi ya mikono yetu utufanyie thabiti, naam, kazi ya mikono yetu uithibitishe.
    (Isisemwe Atukuzwe).

    Ant. Nalitazama mkono wangu wa kuume, nikaona, Ya kuwa hakuna mtu anijuaye.

WIMBO, V. na R. hapana.

    ANT. MAGNIFICAT. Walipokuwa wakila, Yesu alitwaa mkate, akabariki, Akaumega, akawapa wanafunzi wake.
    (Isemwe nzima mwanzo na mwisho pia pasipo kuimhwa.)

Ikiisha DEUS MISEREATUR na Antifona yake, wapige magoti, waseme, Kristo, etc., kama sala ya asubuhi.

Sala ya Usiku

Naungama, etc.
Mwenyezi Mungu, etc.
Bwana Mwenyezi, etc.
ZABURI za kawaida pasipo Antifona.
NUNC DIMITTIS pasipo Antifona.

Ikiisha, wapige magoti, waseme, Kristo, etc., kama sala ya asubuhi.
 

Maundy Thursday

IJUMAA KUU

Leo mwisho wa Masomo, Msomaji asikibusu kitabu wala isisemwe, V. Nawe, BWANA, uturehemu.

Yote kama Alhamisi ya Amri isipokuwa haya,

Sala ya Asubuhi

    ANT. BENEDICTUS. Waliweka juu ya kichwa chake mashitaka yake, yaliyoandikwa, Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.
    (Isemwe nzima mwanzo na mwisho pia.)

Sala ya Jioni

ANT. MAGNIFICAT. Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha; Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.
    (Isemwe nzima mwanzo na mwisho pia pasipo kuimhwa.)
 

Good Friday

MKESHA WA PASAKA

Sala ya Asubuhi

    Yote kama Alhamisi ya Amri isipokuwa,
    ANT. BENEDICTUS. Wanawake wakikaa kwenye kaburi walikuwa wakilia; Wakamwomboleza BWANA.
    (Isemwe nzima mwanzo na mwisho pia.)

Sala ya Adhuhuri

Yote kama Alhamisi ya Amri.

Sala ya Jioni

(Ndiyo ya kwanza ya Pasaka)

Ikiimbwa pamoja na Missa tafuta amri zake katika Missale.

Ikiimbwa kama kawaida ya Sala ya Jioni, inaanzia (zikiisha sala za siri),

    V. Ee Mungu, uwe radhi kutuokoa. Kama kawaida.
    ANT. ZAB. (mwanzo na mwisho) Haleluya, Haleluya, Haleluya.
    ZABURI 117 peke yake.
    1. Enyi mataifa yote, msifuni BWANA; * Enyi watu wote, mhimidini.
    2. Maana fadhili zake kwetu sisi ni kuu; * Na uaminifu wa BWANA ni wa milele.
    Atukuzwe.
    Ant. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
    WIMBO, V. na R. hapana.
    ANT. MAG. (mwanzo na mwisho) Sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi. Haleluya.
    ANT. ZAB. 67 (mwanzo na mwisho) Njia yako etc., na mwishoni, Haleluya.

Ndipo hufuata,

V. BWANA akae nanyi.
R. Pia na roho yako.

Tuombe

Ee Bwana, utumiminie mioyoni mwetu Roho wa upendo wako: Ili sisi sote tuwe na moyo mmoja; kwa kuwa umetushibisha siri zako za Pasaka. Kwa Bwana wetu Yesu Kristo Mwana wako; Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
    V. BWANA akae nanyi.
    R. Pia na roho yako.
    V. Tumhimidi BWANA, Haleluya, Haleluya.
    R. Tumshukuru Mungu. Haleluya, Haleluya.
    Roho zao waaminifu kwa rehema ya Mungu wastarehe katika amani.
    R. Amin.

Sala ya Usiku

Isemwe kama kawaida ya sikuzote, isipokuwa,

    ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
    ZABURI za kawaida. Atukuzwe isemwe.
    WIMBO, SOMO, na VIITIKIO hapana.
    ANT. NUNC DIMITIS. Utuokoe, etc. na mwishoni, Haleluya.

¶ Tangu mwanzo hata mwisho hakuna kupiga magoti Wakati wa Pasaka.
 

Easter Vigil

PASAKA

Sala ya Asubuhi

BADALA ya VENITE

¶ (Sikukuu tu; siyo katika siku nyinginezo saba za Oktavo.)

    1. Pasaka yetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo; * Basi na tuifanye karamu.
    2. Si kwa chachu ya kale wala kwa chachu ya uovu na ubaya; * Bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli.
    3. Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena; * Wala mauti haimtawali tena.
    4. Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; * Lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu.
    5. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, * Na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
    6. Sasa Kristo amefufuka katika wafu, * Limbuko lao waliolala.
    7. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu; * Kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu.
    8. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa; * Kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.
    Atukuzwe.
    ANT. ZAB. Malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni; Akaja akalivingirisha lile jiwe, akalikalia. Haleluya.
    ZABURI Sehemu A. (Kila siku ya Oktavo).
    WIMBO (Badala yake.) 28.
    Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA; * Tutashangilia na kuifurahia.
    V. na R. hapana.
    ANT. BENEDICTUS. Hata alfajiri mapema, siku ya kwanza ya juma, Walikwenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza. Haleluya.
    V. BWANA akae nanyi.
    R. Pia na roho yako.

Tuombe

Sala

V. BWANA akae nanyi.
R. Pia na roho yako.
V. Tumhimidi BWANA, Haleluya, Haleluya.
R. Tumshukuru Mungu, Haleluya, Haleluya.
Roho zao waaminifu, etc.

Sala ya Adhuhuri

WIMBO hapana.
ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
SOMO na VIITIKIO hapana.

Zikiisha Zaburi na Antifona yake,

    Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA; * Tutashangilia na kuifurahia.
    V. BWANA akae nanyi.
    R. Pia na roho yako.

Tuombe

Sala

V. BWANA akae nanyi.
R. Pia na roho yako.
V. Tumhimidi BWANA.
R. Tumshukuru Mungu.
Roho zao waaminifu, etc.

Sala ya Jioni

    ANT. ZAB. Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu. Haleluya.
    WIMBO (Badala yake) 28.
    Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA; * Tutashangilia na kuifurahia.
    V. na R. hapana.
    ANT. MAGNIFICAT. Hata walipotazama, waliona ya kuwa lile jiwe limekwisha kuvingirishwa; Nalo lilikuwa kubwa mno. Haleluya.
    ANT. ZAB. 67. Njia yako, etc., na mwishoni, Haleluya.
    V. BWANA akae nanyi.
    R. Pia na roho yako.

Tuombe

Sala

V. BWANA akae nanyi.
R. Pia na roho yako.
V. Tumhimidi BWANA, Haleluya, Haleluya.
R. Tumshukuru Mungu, Haleluya, Haleluya.
Roho zao waaminifu, etc.

Sala ya Usiku

    ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
    WIMBO, SOMO, na VIITIKIO hapana.
    ANT. NUNC DIMITTIS. Utuokoe, etc., na mwishoni, Haleluya.

Ikiisha Nunc Dimittis na Antifona yake,

    Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA; * Tutashangilia na kuifurahia.
    V. BWANA akae nanyi.
    R. Pia na roho yako.

Tuombe

Sala

V. BWANA akae nanyi.
R. Pia na roho yako.
V. Tumhimidi BWANA.
R. Tumshukuru Mungu.
BWANA Mwenyezi, etc.
 

 

Sikukuu ya Pasaka 1

Mwenyezi Mungu, ulishinda mauti na kutufungulia mlango wa uzima wa milele kwa Mwana wako pekee, Yesu Kristo: Utujalie tuzitimize nadhiri zetu kwa msaada wako; kwa kuwa umezitia mioyoni mwetu kwa neema yako. Kwa Yeye.
 

Easter Day

Jumatatu ya Pasaka 1

Ee Mungu, umeuponya ulimwengu kwa kufufuka kwake Mwana wako Yesu Kristo: Tunakuomba, watu wako wakae na karama zako za mbinguni; ili waustahili uhuru wa uana, na kuufikia uzima wa milele. Kwa Yeye.

Jumanne ya Pasaka 1

Ee Mungu, wapenda sikuzote kuliongeza Kanisa lako kwa kulitilia watu wapya: Uwajalie watumishi wako waambatane na siri ya kufufuka kwake Mwana wako; ili waiitikie siri hiyo kwa matendo kama walivyoikubali kwa imani. Kwa Yeye.

Jumatano ya Pasaka

Ee Mungu, watufurahisha kila mwaka kwa ukumbusho wa kufufuka kwake Bwana wetu: Utujalie, tunakusihi; tustahili kuzifikia furaha za milele kwa Sikukuu hizi tunazozishika hapa duniani. Kwa Yeye.

Alhamisi ya Pasaka

Ee Mungu, umeunganisha kabila za watu mbalimbali kwa kulikiri Jina lako: Uwajalie wote waliozaliwa mara ya pili katika Ubatizo; wawe na umoja wa imani mioyoni mwao, na umoja wa utii katika mwenendo wao. Kwa.

Ijumaa ya Pasaka

Mwenyezi Mungu wa milele, umetupa siri hii ya Pasaka iwe agano la kupatanishwa kwetu nawe: Utujalie, tunakusihi; tuyaige kwa mwenendo wetu mambo hayo tunayoyakiri kwa midomo yetu. Kwa.

Jumamosi ya Pasaka

Mwenyezi Mungu, tunakuomba: Utujalie sisi tulioishika Sikukuu hii ya Pasaka kwa heshima nyingi; tustahili kuzifikia furaha zilizo za milele kwa Sikukuu hiyo. Kwa.
 

Monday in Easter Week

WAKATI WA PASAKA

(Tokea Oktavo ya Pasaka)

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
    UIMBO 29.
    ANT. ZAB. 67. Njia yako, etc., na mwishoni, Haleluya.

Sala ya Asubuhi

ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
WIMBO 30.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Ahimidiwe Mungu Baba,
    Na Mwana mwenye kufufuka,
Na Roho Mfariji naye,
    Zamani, leo, na milele. Amin.

    ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
    SOMO. Sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. BWANA amefufuka kweli kweli. Haleluya. Haleluya.
    R. BWANA amefufuka kweli kweli. Haleluya. Haleluya.
    V. Naye amemtokea Simoni.
    R. Haleluya. Haleluya.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. BWANA amefufuka kweli kweli. Haleluya. Haleluya.
    V. Wale wanafunzi wakafurahi. Haleluya.
    R. Walipomwoma BWANA. Haleluya.

Ibada isemwe hivyo Wakati wa Pasaka hata Mkesha wa Kupaa, kila siku, isipokuwa ni Sikukuu.

Sala ya Ukumbusho wa Msalaba (M)

    Ant. Aliyesulibiwa amefufuka katika wafu; Na kutukomboa sisi. Haleluya.
    V. Semeni katika mataifa. Haleluya.
    R. BWANA ametamalaki. Haleluya.

Tuombe

Ee Mungu, ulikubali Mwana wako auvumilie Msalaba kwa ajili yetu, azifukuzie mbali nasi nguvu zote za adui: Utukirimie sisi, watumishi wako; tuwe na neema ya kufufuliwa katika wafu. Kwa Yeye.
 

Easter Season

(actually the Octave of Easter)

S. B. I Pasaka

Baba Mwenyezi, ulimtoa Mwana wako pekee afe kwa ajili ya dhambi zetu, na kufufuka tupate kufanyizwa wema: Utujalie tuitupie mbali chachu ya uovu na ubaya; ili tupate kukutumikia sikuzote kwa usafi wa imani na mwenendo. Kwa Yeye.
 

1st Sunday after Easter

S. B. II Pasaka

Mwenyezi Mungu, ulimtoa Mwana wako awe kwetu dhabihu kwa dhambi na mfano wa wema: Utujalie neema tuifahamu sikuzote kwa shukrani fadhili yake iliyo bora; tujitahidi kila siku kuzifuata nyayo zake takatifu. Kwa Yeye.
 

2 Easter

J5 Yusufu, Mfadhili wa Kanisa Katholiko, 1.
Kama Machi 19, Wakati wa Pasaka.
 

St. Joseph

S. B. III Pasaka

Mwenyezi Mungu, umewaonyesha wanaopotea nuru ya kweli yako, wapate kuirudia njia ya haki: Uwajalie wote walioingizwa katika ushirika wa dini ya Kristo; wayakatae yasiyopatana na jina hilo, na kuyafuata yanayopatana nalo. Kwa Yeye.
 

3 Easter

S. B. IV Pasaka

Mwenyezi Mungu, Wewe peke yako waweza kuzitawala nia kaidi za wenye dhambi: Uwajalie watu wako wayapende uliyoyaamuru, na kuyataka uliyoyaahidi; ili, katika dunia hii isiyo starehe, mioyo yetu istarehe huko kunako furaha za kweli. Kwa.
 

4 Easter

S. B. V Pasaka

Ee Mungu, uliye asili ya mema yote: Utujalie tuyaombayo; uziangaze nia zetu, ili tuyawaze yaliyo ya haki, na kutuelekeza mioyo hata tuyatimize. Kwa.
 

5 Easter

KUPAA KWA BWANA

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni Atakuja jinsi iyo hiyo. Haleluya.
    ZABURI Sehemu A. (Sikukuu, na S. B.).
    WIMBO 31.
    ANT. ZAB. 67. Njia yako, etc., na mwishoni, Haleluya.

Sala

Mwenyezi Mungu, tunasadiki ya kwamba Bwana wetu Yesu Kristo, Mwana wako pekee, amepaa mbinguni: Utujalie na sisi tupae huko kwa moyo na akili; na kukaa pamoja naye sikuzote katika mambo ya mbinguni. Kwa Yeye.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Bwana, baada ya kusema nao, alichukuliwa juu mbinguni; Akaketi mkono wa kuume wa Mungu. Haleluya.
    WIMBO 32.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Uliyeshinda, ukapaa,
    Ee Yesu, twakusifu sana,
Pamoja naye Mungu Baba,
    Na Mungu Roho Mtakatifu. Amin.

    ANT. ZAB. Haleluya, Haleluya, Haleluya.
    SOMO. Watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni; atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Kristo amepaa juu. Haleluya. Haleluya.
    R. Kristo amepaa juu. Haleluya. Haleluya.
    V. Ameteka mateka.
    R. Haleluya. Haleluya.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Kristo amepaa juu. Haleluya. Haleluya.
    V. Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu. Haleluya.
    R. Kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu. Haleluya.

Sala ya Ukumbusho wa Kupaa

    Ant. Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu; Kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu. Haleluya.
    V. Mungu amepaa kwa kelele za shangwe. Haleluya.
    R. BWANA kwa sauti ya baragumu. Haleluya.
 

Ascension Day

S. B. ya Kupaa

Ee Mungu, Mfalme wa utukufu, ulimpandisha kwa shangwe Mwana wako pekee Yesu Kristo katika ufalme wako wa mbinguni: Usituache yatima; bali utupelekee Roho wako Mtakatifu, atufariji, na kutupandisha huko alikotangulia Mwokozi wetu Kristo. Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

Sunday after the Ascension

Ijumaa na Mkesha wa Pentekote
Kama S. B. ya Kupaa
 

Friday & Vigil of Pentecost

PENTEKOTE

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine; Roho wa kweli. Haleluya.
    ZABURI Sehemu A. (Kila siku ya Oktavo).
    WIMBO 33.
    ANT. ZAB. 67. Njia yako, etc., na mwishoni, Haleluya.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Mitume wakasema kwa lugha nyingine Matendo makuu ya Mungu. Haleluya.
    WIMBO 34.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Ahimidiwe Mungu Baba,
    Na Mwana mwenye kufufuka,
Na Roho Mfariji naye,
    Zamani, leo, na milele. Amin.

    ANT. ZAB Haleluya, Haleluya, Haleluya
    SOMO. Basi sauti hii ilipokuja makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Huyu Msaidizi ndiye Roho Mtakatifu. Haleluya, Haleluya.
    R. Huyu Msaidizi ndiye Roho Mtakatifu. Haleluya, Haleluya.
    V. Yeye atawafundisha yote.
    R. Haleluya, Haleluya.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Huyu Msaidizi ndiye Roho Mtakatifu. Haleluya, Haleluya.
    V. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu. Haleluya.
    R. Wakaanza kusema. Haleluya.
 

Pentecost (Whitsunday)

Sikukuu ya Pentekote I

Ee Mungu, kama majira haya, uliwafundisha mioyo yao wenye imani kwa nuru ya Roho Mtakatifu: Utujalie kwa Roho huyo tuyajue mambo yote kwa akili; na kuifurahia sikuzote faraja yake takatifu. Kwa Bwana wetu Yesu Kristo Mwana wako; Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

Day of Pentecost

Jumatatu ya Pentekote I

Ee Mungu, uliwapa Mitume wako Roho Mtakatifu: Uwajalie watu wako mazao ya maombi yao yenye ibada; ili wale uliowapa imani wakirimiwe nawe amani pia. Kwa Bwana wetu Yesu Kristo Mwana wako; Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Jumanne ya Pentekote I

Ee Mungu, tunakuomba: Nguvu za Roho Mtakatifu ziwe pamoja nasi; zitusafishe mioyo yetu kwa neema yake, na kutulinda na mambo yote yanayotupinga. Kwa Bwana wetu Yesu Kristo Mwana wako; Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

Monday of the Week of Pentecost

Jumatano, Robo Mwaka

Ee Bwana, tunakusihi: Mfariji atokaye kwako atuangaze nia zetu; na kutuongoza katika kweli yote, kama vile Mwana wako alivyoahidi. Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Siku ya Alhamisi itumike sala ya Sikukuu ya Pentekote.

Ijumaa, Robo Mwaka

Ee Mungu, mwenye rehema, uzisikilize dua za Kanisa lako: Uliweke salama katika umoja wa Roho Mtakatifu; lisisumbuliwe kwa mapigano ya adui ye yote. Kwa Bwana wetu Yesu Kristo Mwana wako; Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Jumamosi, Robo Mwaka

Ee Bwana, tunakusihi: Utumiminie mioyoni mwetu Roho wako Mtakatifu; ili tulivyoumbwa kwa hekima yake, vivyo hivyo tutawaliwe kwa maongozi yake. Kwa Bwana wetu Yesu Kristo Mwana wako; Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Sala ya Adhuhuri, Jumamosi, ndiyo mwisho wa Wakati wa Pasaka.
 

Wednesday, Ember Days

UTATU MTUKUFU

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Utukufu una Wewe, Utatu uliye Uungu mmoja; Tangu milele, na sasa, na hata milele.
    ZABURI Sehemu A. (Sikukuu tu).
    WIMBO 35.

Sala

Mwenyezi Mungu wa milele, umetupa sisi watumishi wako neema, katika imani ya kweli, kuutambua utukufu wa Utatu wa milele, na katika uweza wa Enzi ya Uungu kuuabudu Umoja: Utujalie, tunakusihi; tulindwe daima na adui zetu, kwa uthabiti wa imani hiyo. Kwa.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, Hata milele na milele.
    WIMBO 36.

Sala ya Adhuhuri

    SOMO. Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nasi sote sasa na milele.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Ee BWANA, umehimidiwa, katika anga la mbinguni.
    R. Ee BWANA, umehimidiwa, katika anga la mbinguni.
    V. Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
    R. Katika anga la mbinguni.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Ee BWANA, umehimidiwa, katika anga la mbinguni.
    V. Jina la BWANA lihimidiwe.
    R. Tangu leo na hata milele.
 

Trinity

S. B. I Pentekote

Ee Mungu, uliye uwezo wao wakutumainio, pasipo Wewe udhaifu wetu wa kibinadamu haufai kitu: Uzikubali kwa rehema dua zetu; utujalie tukupendeze kwa kuzikubali amri zako, na kuzitimiza kwa moyo wote. Kwa.

Baada ya Sikukuu ya Utatu Mt. hata Majilio Ibada ndiyo ya kawaida, isipokuwa ni Sikukuu.
 

1 Pentecost (Trinity Sunday)

MWILI MTUKUFU WA KRISTO

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Kuhani wa milele kwa mfano wa Melkizedeki, Kristo aliye BWANA, Alileta mkate na divai. Haleluya.
    ZABURI Sehemu A. (Sikukuu, na S. B.).
    WIMBO 37.

Sala

Ee Mungu, umetuachia ukumbusho wa Mateso yako katika Sakramenti iliyo ya ajabu: Utujalie, tunakusihi, tuziheshimu siri takatifu za Mwili na Damu yako; ili tuyaone daima ndani yetu mazao ya ukombozi wako. Uishiye na kumiliki pamoja na Mungu Baba, katika umoja wa Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Uliwalisha watu wako chakula cha mashujaa; Ukawaandalia mkate utokao mbinguni. Haleluya.
    WIMBO 38.

Sala ya Adhuhuri

Ubeti wa mwisho wa Wimbo.

Ee Yesu, Mwana wa Bikira,
    Twakutolea sifa zetu,
Pamoja naye Mungu Baba,
    Na Mungu Roho Mtakatifu. Amin.

    SOMO. Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate, na akiisha kushukuru akaumega, akasema: Huu. ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Aliwalisha kwa unono wa ngano. Haleluya, Haleluya.
    R. Aliwalisha kwa unono wa ngano. Haleluya, Haleluya.
    V. Akawashibisha kwa asali itokayo mwambani.
    R. Haleluya, Haleluya.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Aliwalisha kwa unono wa ngano. Haleluya. Haleluya.
    V. Ulitoa mkate katika nchi. Haleluya.
    R. Na divai imfurahishe mtu moyo wake. Haleluya.

Sala ya Ukumbusho wa Mwili wa Kristo

    Ant. Ee ajabu ya wema wa Roho wako, BWANA! unawapa watoto wako chakula bora cha mbinguni, ili uwaonyeshe wema wako; Wenye njaa unawashibisha mema; na wenye mali walioshiba unawaondoa mikono mitupu. Haleluya.
    V. Aliwapa nafaka ya mbinguni. Haleluya.
    R. Mwanadamu akala chakula cha mashujaa. Haleluya.
 

Corpus Christi

S. B. II Pentekote

Ee Bwana, hukosi kuwatawala watu unaowalea daima kwa pendo lako: Utulinde, tunakusihi, chini ya himaya ya tunza lako jema; ututie hofu na pendo lisilokoma la Jina lako takatifu. Kwa.
 

2 Pentecost

MOYO MTAKATIFU WA YESU

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, Nami nitawapumzisha.
    ZABURI Sehemu A. (Sikukuu tu).
    WIMBO 39.

Sala

Ee Mungu, umetupa kwa rehema zako upendo usiopimika katika Moyo wake Mwana wako uliojeruhi kwa dhambi zetu: Utujalie, tunakusihi; tumtolee ibada yetu ya utauwa, na kumwonyesha shukrani itupasavyo. Kwa Yeye.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Yesu alisimama, akapaza sauti yake, akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
    WIMBO 39.

Sala ya Adhuhuri

    SOMO. Nampigia Baba magoti, ambaye kwa Jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa, awajalieni, kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake, kufanywa imara kwa nguvu, kwa. kazi ya Roho wake, katika mtu wa ndani; Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Nalisema, Ee BWANA, unifadhili.
    R. Nalisema, Ee BWANA, unifadhili.
    V. Uniponye roho yangu, maana nimekutenda dhambi.
    R. Unifadhili.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Nalisema, Ee BWANA, unifadhili.
    V. Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu.
    R. Amewapa wamchao chakula.

Sala ya Ukumbusho wa Moyo Mt.

    Ant. Walipomjia Yesu, na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu; Lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki, na mara ikatoka damu na maji.
    V. Kwa furaha mtateka.
    R. Visimani mwa wokovu.
 

Sacred Heart of Jesus

S. B. III Pentekote

Ee Mungu, Mlinzi wao wote wakuaminio, pasipo Wewe hakuna nguvu, hakuna utakatifu: Utuzidishie rehema zako; ili sisi, tulio nawe kuwa Mtawala na Kiongozi wetu, tuyapitie mambo yenye mwisho, yasije yakatupotea mambo yasiyo na mwisho. Kwa.
 

3 Pentecost

S. B. IV Pentekote

Ee Bwana, tunakusihi: Uyaongoze mambo ya ulimwengu huu; ili sisi tuwe na amani, na Kanisa lako lipate furaha kwa kukuabudu katika utulivu. Kwa.
 

4 Pentecost

S. B. V Pentekote

Ee Mungu, umewawekea wakupendao mema yapitayo akili za wanadamu: Utumiminie mioyoni mwetu pendo lako; ili sisi tukupende Wewe katika yote na kuliko yote, na kuzipata ahadi zako zipitazo haja zetu zote. Kwa.
 

5 Pentecost

S. B. VI Pentekote

Ee Mungu, Mwenye uweza wote, kwako Wewe hutoka yote yaliyo bora: Utumiminie mioyoni mwetu pendo lako, tulipende Jina lako na kuongezewa roho ya ibada; uyazidishe yaliyo mema ndani yetu, na kuyahifadhi kwa tunza lako la Ubaba. Kwa.
 

6 Pentecost

S. B. VII Pentekote

Ee Mungu, tunza lako halikosi kuuongoza ulimwengu mzima: Tunakusihi kwa unyenyekevu; utuondolee madhara yote, na kutuletea mambo yote ya kutufaa. Kwa.
 

7 Pentecost

S. B. VIII Pentekote

Ee Bwana, pasipo Wewe hatuwezi neno lo lote lililo jema: Tunakusihi; utukirimie sikuzote moyo wa kuyafikiri yaliyo mema, na kuyatenda, ili tuwe na nguvu ya kuenenda kama upendavyo. Kwa.
 

8 Pentecost

S. B. IX Pentekote

Ee Bwana, tunakusihi: Uyatege masikio yako ya rehema kwa sala zao wakuombao; uwape moyo wa kuyataka uyapendayo, ili uwajalie haja zao wakuombapo. Kwa.
 

9 Pentecost

S. B. X Pentekote

Ee Mungu, wazionyesha nguvu zako zisizo na kiasi hasa kwa kuachilia na kurehemu: Utuzidishie rehema zako; ili, tukizikimbilia ahadi zako, tuyashiriki mema ya mbinguni. Kwa.
 

10 Pentecost

S. B. XI Pentekote

Mwenyezi Mungu, wa milele, kwa wema wako mwingi wa Ubaba watupa karama za kupita stahili zetu na dua zetu: Utumiminie rehema zako; ili tusamehewe makosa yaitishayo mioyo yetu, na kupewa baraka zako sala zetu zisizozistahili. Kwa.
 

11 Pentecost

S. B. XII Pentekote

Mwenyezi Mungu, mwenye rehema, watu wako wakuaminio hukutumikia vema na amini kwa karama yako tu: Utujalie, tunakusihi; tusijikwae po pote, bali tuzifikie ahadi zako za mbinguni. Kwa.
 

12 Pentecost

S. B. XIII Pentekote

Mwenyezi Mungu, wa milele: Utuzidishie imani, tumaini, na upendo; utupe moyo wa kuyapenda uliyoyaamuru, ili tuyapate uliyoyaahidi. Kwa.
 

13 Pentecost

S. B. XIV Pentekote

Ee Bwana, pasipo Wewe udhaifu wetu wa kibinadamu huteleza: Tunakusihi, ulilinde Kanisa lako kwa neema yako ya daima; ukalisaidie liokolewe na madhara, na kuongozwa kwenye mambo ya wokovu. Kwa.
 

14 Pentecost

S. B. XV Pentekote

Ee Bwana, tunakusihi: Huruma yako ya daima ilitakase Kanisa lako na kulilinda; na kwa kuwa pasipo Wewe haliwezi kukaa salama, liongozwe sikuzote kwa msaada wa wema wako. Kwa.
 

15 Pentecost

S. B. XVI Pentekote

Ee Bwana, tunakusihi: Utujalie neema yako; itutangulie sikuzote na kutufuata, ili kututia moyo wa bidii wa kutenda kazi zilizo njema. Kwa.
 

16 Pentecost

S. B. XVII Pentekote

Ee Bwana, hakuna Mungu ila Wewe: Tunakusihi; uwajalie watu wako wayaepuke mambo yote ya kishetani, ili wakufuate Wewe kwa mioyo safi. Kwa.
 

17 Pentecost

Robo Mwaka
(baada ya Septemba 14)

Jumatano

Ee Bwana, tunakusihi, uzisikie dua zetu: Huruma zako zituwie dawa ya udhaifu wetu; ili tulivyojiharibu kwa dhambi zetu, tutengenezwe kwa rehema zako. Kwa.

Ijumaa

Mwenyezi Mungu, tunakusihi: Uisikie dua yetu; ili tuifulize ibada ya siku hii ya leo, na kukupendeza kwa mwili na kwa roho. Kwa.

Jumamosi

Mwenyezi Mungu, wa milele, unatuletea afya ya mwili na roho kwa njia ya kujinyima kwetu: Tunakusihi kwa unyenyekevu; utukubali katika kufunga kwetu na kusali kwetu, na kutujalia msaada wako sasa na siku zijazo. Kwa.
 

Ember Days

S. B. XVIII Pentekote

Ee Bwana, pasipo msaada wako hatuwezi kukupendeza: Tunakusihi; utuonyeshe uweza wa huruma zako, ili Roho wako Mtakatifu aiongoze mioyo yetu. Kwa Bwana wetu Yesu Kristo Mwana wako; Aishiye na kumiliki pamoja nawe, katika umoja wake Yeye huyo Roho Mtakatifu, Mungu daima milele na milele. Amin.
 

18 Pentecost

S. B. XIX Pentekote

Mwenyezi Mungu, mwenye rehema: Utuondolee kwa neema yako mambo yote yanayatupinga; ili tuwe tayari, miili na roho, kuzitimiza kazi zako kwa mioyo iliyotulia. Kwa.
 

19 Pentecost

S. B. XX Pentekote

Ee Bwana, tunakusihi: Uwakirimie watu wako wakuaminio samaha na amani; ili watakaswe na machukizo yote, na kukutumikia kwa mioyo isiyoshughulika. Kwa.
 

20 Pentecost

S. B. XXI Pentekote

Ee Bwana, tunakusihi: Uulinde ujamaa wako kwa pendo lako la daima; ili uponywe kwa himaya yako katika shida zote, na kulitumikia Jina lako kwa matendo mema. Kwa.
 

21 Pentecost

S. B. XXII Pentekote

Ee Mungu, Wewe ndiwe kimbilio letu na nguvu zetu, asili ya utakatifu wote: Uzikubali sala takatifu za Kanisa lako; utujalie tuyapate yote tunayoyaomba kwa imani. Kwa.
 

22 Pentecost

S. B. XXIII Pentekote

Ee Bwana, unatuona tumejifungia dhambi kwa udhaifu wetu: Tunakusihi; uyasamehe makosa ya watu wako, ili kwa wema wako tufunguliwe katika vifungo vyetu. Kwa.

Ikiwa S. B. baada ya Pentekote zimezidi, zitumike sala za S. B. baada ya Ufunuo zilizoachwa. Tafuta habari yake katika Kalendari ya Mwaka. Na sala hii ifuatayo itumike sikuzote S. B. Kabla ya Majilio.
 

23 Pentecost

S. B. Kabla ya Majilio

Ee Bwana, tunakusihi: Uiamshe mioyo ya watu wako wakuaminio; ili wayatamani mazao ya neema yako, na kuzidi kuuona msaada wako wa Ubaba. Kwa.
 

Sunday before Advent

KUTABARUKU KANISA

Sala ya Jioni (ya 1 na ya 2)

    ANT. ZAB. Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala, Kwa mataifa yote.
    ZABURI Sehemu A. (Sikukuu tu).
    WIMBO 40.

Sala

Ee Mungu, wapenda kila mwaka kutuleta salama kwa Sikukuu ya ukumbusho wa kulitabaruku Kanisa letu [Kuu], ili tuzihudhurie siri zako: Utusikie sisi tulio watu wako; kila mtu atakayeomba baraka katika Kanisa hilo, apate ayatakayo na kuyafurahia. Kwa.

Sala ya Asubuhi

    ANT. ZAB. Bila shaka hapa ni nyumba ya Mungu, Na hili ni lango la mbinguni.
    WIMBO 41.

Sala ya Adhuhuri

    SOMO. Nilisikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikisema, Tazama, maskani ya Mungu i pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake; naye mwenyewe, Mungu pamoja nao, atakuwa Mungu wao.
    R. Tumshukuru Mungu.
    V. Hapa ni patakatifu asalipo Kasisi.
    R. Hapa ni patakatifu asalipo Kasisi.
    V. Kwa ajili ya dhambi na makosa ya watu
    R. Asalipo Kasisi.
    V. Atukuzwe, etc.
    R. Hapa ni patakatifu asalipo Kasisi.
    V. Hii ndiyo nyumba ya BWANA, imejengwa imara.
    R. Msingi wake u juu ya mwamba ulio thabiti.

Sala ya Ukumbusho

    Ant. Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ni nyumba ya Mungu, na hili ni lango la mbinguni.
    V. Utakatifu ndio uifaao nyumba yako.
    R. Ee BWANA, milele na milele.

Dedication of a Church

 

Return to the Zanzibar Prayer Book

Web author: Charles Wohlers U. S. EnglandScotlandIrelandWalesCanadaWorld